Luanda

Article in other languages:

Jiji la Luanda
Nchi Angola
Luanda katika Angola
Luanda inavyoonekana kutoka angani
Luanda (Juni 2005)

Luanda (pia São Paulo de Luanda au Loanda) ni mji mkuu pia mji mkubwa wa Angola ikiwa na wakazi 2.776.125 (2005).

Yaliyomo

Jiografia

Mji wa Luanda uko mkoani Luanda kaskazini ya mdomo wa mto Cuanza mwambaoni ya Atlantiki.


Wakazi

Kati ya wakazi milioni 2,7 walio wengi kabisa ni Waafrika wa makabila kama vile Waovimbundu, Wakimbundu na Wakongo. Lugha rasmi ni Kireno lakini lugha nyingi za kibantu zinatumika pia.


Historia

Mji ulianzishwa mwaka 1575 BK na Wareno kwa jina la São Paulo de Luanda. Imekuwa mji mkuu wa Angola tangu 1627. Hadi 1850 Luanda ilikuwa kitovu cha biashara ya watumwa kwenda Brazil.

Wakati wa uhuru mwaka 1975 wakazi wengi Wareno waliondoka mjini. Vita ya wenyewe kwa wenyewe katika Angola kati ya 1974 - 2002 ilileta hasara pia kwa ajili ya mji mkuu.

Uchumi

Luanda ni bandari muhimu nchini pia mwanzo wa reli kwenda Malange.

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Questions for article: angola africa luanda, angola africa luanda portuguese, atlantico azul imbondex, bahia de luanda, 罗安达(luanda), Фото Луанда, flights from luanda angola to freetown sierra leone, flights from luanda to nairobi, fortaleza são pedro angola, historias imbondex comercio geral, imagens de luanda antigamente

This article is from Wikipedia. All text is available under the terms of the GNU Free Documentation License.


IHS Europe: Infrared Heating Systems for Home and Business.